HABARI MPYA

Monday, December 3, 2012

NAPE: VIGOGO CHADEMA WANA KADI ZA CCM




*Wengine wanaendelea kuzilipia mpaka leo
*Ahoji Dk. Slaa kairudisha lini na wapi?
*Awaita waganga njaa si wanasiasa


MWANZA,TANZANIA
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenez Nape Nnauye, amerusha kombora kuwa vigogo wengi ndani ya CHADEMA wameendelea kuwa na kadi za CCM na wengine wanaendelea kuzilipia, jambo linalothibitisha unafiki walionao viongozi wengi wa upinzani nchini.

Akifungua mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya Nyamagana, jijini Mwanza, leo uliokuwa na lengo la kupokea maazimio ya Mkutano Mkuu wa nane wa CCM na hotuba ya Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Jakaya Kikwete, Nape amedai siasa kwa sasa imevamiwa na makanjanja wengi ambao kazi yao ni kuganga njaa na hivyo huishi kinafiki kwakuwa wakisemacho sicho wanachokiishi.

Sambamba na kombora hilo, Nape ameitaka CCM kuhakikisha inatoa uongozi mzuri ili kudhibiti uvamizi huu wa makanjanja kwenye siasa za hapa nchini. SOMA ZAIDI

No comments:

Post a Comment